Swahili - Sorah Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder)

Noble Quran » Swahili » Sorah Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder)

Choose the reader


Swahili

Sorah Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Verses Number 25
إِذَا السَّمَاءُ انشَقَّتْ ( 1 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 1
Itapo chanika mbingu,
وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ ( 2 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 2
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
وَإِذَا الْأَرْضُ مُدَّتْ ( 3 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 3
Na ardhi itakapo tanuliwa,
وَأَلْقَتْ مَا فِيهَا وَتَخَلَّتْ ( 4 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 4
Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,
وَأَذِنَتْ لِرَبِّهَا وَحُقَّتْ ( 5 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 5
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
يَا أَيُّهَا الْإِنسَانُ إِنَّكَ كَادِحٌ إِلَىٰ رَبِّكَ كَدْحًا فَمُلَاقِيهِ ( 6 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 6
Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.
فَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ بِيَمِينِهِ ( 7 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 7
Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,
فَسَوْفَ يُحَاسَبُ حِسَابًا يَسِيرًا ( 8 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 8
Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,
وَيَنقَلِبُ إِلَىٰ أَهْلِهِ مَسْرُورًا ( 9 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 9
Na arudi kwa ahali zake na furaha.
وَأَمَّا مَنْ أُوتِيَ كِتَابَهُ وَرَاءَ ظَهْرِهِ ( 10 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 10
Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,
فَسَوْفَ يَدْعُو ثُبُورًا ( 11 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 11
Basi huyo ataomba kuteketea.
وَيَصْلَىٰ سَعِيرًا ( 12 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 12
Na ataingia Motoni.
إِنَّهُ كَانَ فِي أَهْلِهِ مَسْرُورًا ( 13 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 13
Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.
إِنَّهُ ظَنَّ أَن لَّن يَحُورَ ( 14 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 14
Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.
بَلَىٰ إِنَّ رَبَّهُ كَانَ بِهِ بَصِيرًا ( 15 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 15
Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!
فَلَا أُقْسِمُ بِالشَّفَقِ ( 16 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 16
Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,
وَاللَّيْلِ وَمَا وَسَقَ ( 17 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 17
Na kwa usiku na unavyo vikusanya,
وَالْقَمَرِ إِذَا اتَّسَقَ ( 18 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 18
Na kwa mwezi unapo pevuka,
لَتَرْكَبُنَّ طَبَقًا عَن طَبَقٍ ( 19 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 19
Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka!
فَمَا لَهُمْ لَا يُؤْمِنُونَ ( 20 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 20
Basi wana nini hawaamini?
وَإِذَا قُرِئَ عَلَيْهِمُ الْقُرْآنُ لَا يَسْجُدُونَ ۩ ( 21 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 21
Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu?
بَلِ الَّذِينَ كَفَرُوا يُكَذِّبُونَ ( 22 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 22
Bali walio kufuru wanakanusha tu.
وَاللَّهُ أَعْلَمُ بِمَا يُوعُونَ ( 23 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 23
Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria.
فَبَشِّرْهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ ( 24 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 24
Basi wabashirie adhabu chungu!
إِلَّا الَّذِينَ آمَنُوا وَعَمِلُوا الصَّالِحَاتِ لَهُمْ أَجْرٌ غَيْرُ مَمْنُونٍ ( 25 ) Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Ayaa 25
Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika.

Random Books

Choose language

Choose Sorah

Random Books

Choose tafseer

Participate

Bookmark and Share