Swahili - Sorah Ad-Dukhan ( The Smoke )

Noble Quran » Swahili » Sorah Ad-Dukhan ( The Smoke )

Choose the reader


Swahili

Sorah Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Verses Number 59
حم ( 1 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 1
H'a Mim
وَالْكِتَابِ الْمُبِينِ ( 2 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 2
Naapa kwa Kitabu kinacho bainisha,
إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةٍ مُّبَارَكَةٍ ۚ إِنَّا كُنَّا مُنذِرِينَ ( 3 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 3
Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.
فِيهَا يُفْرَقُ كُلُّ أَمْرٍ حَكِيمٍ ( 4 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 4
Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima,
أَمْرًا مِّنْ عِندِنَا ۚ إِنَّا كُنَّا مُرْسِلِينَ ( 5 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 5
Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma.
رَحْمَةً مِّن رَّبِّكَ ۚ إِنَّهُ هُوَ السَّمِيعُ الْعَلِيمُ ( 6 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 6
Ni rehema itokayo kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ni Mwenye kusikia Mwenye kujua.
رَبِّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا ۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ ( 7 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 7
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, ikiwa nyinyi mna yakini.
لَا إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ يُحْيِي وَيُمِيتُ ۖ رَبُّكُمْ وَرَبُّ آبَائِكُمُ الْأَوَّلِينَ ( 8 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 8
Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo.
بَلْ هُمْ فِي شَكٍّ يَلْعَبُونَ ( 9 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 9
Lakini wao wanacheza katika shaka.
فَارْتَقِبْ يَوْمَ تَأْتِي السَّمَاءُ بِدُخَانٍ مُّبِينٍ ( 10 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 10
Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapo leta moshi ulio dhaahiri,
يَغْشَى النَّاسَ ۖ هَٰذَا عَذَابٌ أَلِيمٌ ( 11 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 11
Utakao wafunika watu: Hii ni adhabu chungu!
رَّبَّنَا اكْشِفْ عَنَّا الْعَذَابَ إِنَّا مُؤْمِنُونَ ( 12 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 12
Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini.
أَنَّىٰ لَهُمُ الذِّكْرَىٰ وَقَدْ جَاءَهُمْ رَسُولٌ مُّبِينٌ ( 13 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 13
Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwisha wafikia Mtume mwenye kubainisha.
ثُمَّ تَوَلَّوْا عَنْهُ وَقَالُوا مُعَلَّمٌ مَّجْنُونٌ ( 14 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 14
Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu.
إِنَّا كَاشِفُو الْعَذَابِ قَلِيلًا ۚ إِنَّكُمْ عَائِدُونَ ( 15 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 15
Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!
يَوْمَ نَبْطِشُ الْبَطْشَةَ الْكُبْرَىٰ إِنَّا مُنتَقِمُونَ ( 16 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 16
Siku tutayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa.
وَلَقَدْ فَتَنَّا قَبْلَهُمْ قَوْمَ فِرْعَوْنَ وَجَاءَهُمْ رَسُولٌ كَرِيمٌ ( 17 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 17
Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu.
أَنْ أَدُّوا إِلَيَّ عِبَادَ اللَّهِ ۖ إِنِّي لَكُمْ رَسُولٌ أَمِينٌ ( 18 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 18
Akasema: Nipeni waja wa Mwenyezi Mungu; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu.
وَأَن لَّا تَعْلُوا عَلَى اللَّهِ ۖ إِنِّي آتِيكُم بِسُلْطَانٍ مُّبِينٍ ( 19 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 19
Na msimfanyie kiburi Mwenyezi Mungu; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi.
وَإِنِّي عُذْتُ بِرَبِّي وَرَبِّكُمْ أَن تَرْجُمُونِ ( 20 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 20
Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe.
وَإِن لَّمْ تُؤْمِنُوا لِي فَاعْتَزِلُونِ ( 21 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 21
Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami.
فَدَعَا رَبَّهُ أَنَّ هَٰؤُلَاءِ قَوْمٌ مُّجْرِمُونَ ( 22 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 22
Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu.
فَأَسْرِ بِعِبَادِي لَيْلًا إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ ( 23 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 23
Mwenyezi Mungu akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa.
وَاتْرُكِ الْبَحْرَ رَهْوًا ۖ إِنَّهُمْ جُندٌ مُّغْرَقُونَ ( 24 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 24
Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo zamishwa.
كَمْ تَرَكُوا مِن جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ ( 25 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 25
Mabustani mangapi, na chemchem ngapi waliziacha!
وَزُرُوعٍ وَمَقَامٍ كَرِيمٍ ( 26 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 26
Na mimea na vyeo vitukufu!
وَنَعْمَةٍ كَانُوا فِيهَا فَاكِهِينَ ( 27 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 27
Na neema walizo kuwa wakijistareheshea!
كَذَٰلِكَ ۖ وَأَوْرَثْنَاهَا قَوْمًا آخَرِينَ ( 28 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 28
Ndio hivyo! Na tukawarithisha haya watu wenginewe.
فَمَا بَكَتْ عَلَيْهِمُ السَّمَاءُ وَالْأَرْضُ وَمَا كَانُوا مُنظَرِينَ ( 29 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 29
La mbingu wala ardhi hazikuwalilia, wala hawakupewa muhula.
وَلَقَدْ نَجَّيْنَا بَنِي إِسْرَائِيلَ مِنَ الْعَذَابِ الْمُهِينِ ( 30 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 30
Na bila ya shaka tuliwaokoa Wana wa Israili katika adhabu ya kuwadhalilisha,
مِن فِرْعَوْنَ ۚ إِنَّهُ كَانَ عَالِيًا مِّنَ الْمُسْرِفِينَ ( 31 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 31
Ya Firauni. Hakika yeye alikuwa jeuri katika wenye kupindukia mipaka.
وَلَقَدِ اخْتَرْنَاهُمْ عَلَىٰ عِلْمٍ عَلَى الْعَالَمِينَ ( 32 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 32
Na tuliwakhiari kwa ujuzi wetu kuliko walimwengu wenginewe.
وَآتَيْنَاهُم مِّنَ الْآيَاتِ مَا فِيهِ بَلَاءٌ مُّبِينٌ ( 33 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 33
Na tukawapa katika ishara zenye majaribio yaliyo wazi.
إِنَّ هَٰؤُلَاءِ لَيَقُولُونَ ( 34 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 34
Hakika hawa wanasema:
إِنْ هِيَ إِلَّا مَوْتَتُنَا الْأُولَىٰ وَمَا نَحْنُ بِمُنشَرِينَ ( 35 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 35
Hapana ila kufa kwetu mara ya kwanza tu, wala sisi hatufufuliwi.
فَأْتُوا بِآبَائِنَا إِن كُنتُمْ صَادِقِينَ ( 36 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 36
Basi warudisheni baba zetu, ikiwa nyinyi mnasema kweli.
أَهُمْ خَيْرٌ أَمْ قَوْمُ تُبَّعٍ وَالَّذِينَ مِن قَبْلِهِمْ ۚ أَهْلَكْنَاهُمْ ۖ إِنَّهُمْ كَانُوا مُجْرِمِينَ ( 37 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 37
Je! Ni wao bora au watu wa Tubbaa' na walio kuwa kabla yao? Tuliwaangamiza. Hakika hao walikuwa wakosefu.
وَمَا خَلَقْنَا السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ وَمَا بَيْنَهُمَا لَاعِبِينَ ( 38 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 38
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo baina yake kwa mchezo.
مَا خَلَقْنَاهُمَا إِلَّا بِالْحَقِّ وَلَٰكِنَّ أَكْثَرَهُمْ لَا يَعْلَمُونَ ( 39 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 39
Hatukuviumba hivyo ila kwa Haki, lakini wengi wao hawajui.
إِنَّ يَوْمَ الْفَصْلِ مِيقَاتُهُمْ أَجْمَعِينَ ( 40 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 40
Hakika siku ya Uamuzi ni wakati ulio wekwa kwa wao wote.
يَوْمَ لَا يُغْنِي مَوْلًى عَن مَّوْلًى شَيْئًا وَلَا هُمْ يُنصَرُونَ ( 41 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 41
Siku ambayo rafiki hatamfaa rafiki yake kwa chochote, wala hawatanusuriwa.
إِلَّا مَن رَّحِمَ اللَّهُ ۚ إِنَّهُ هُوَ الْعَزِيزُ الرَّحِيمُ ( 42 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 42
Isipo kuwa atakaye mrehemu Mwenyezi Mungu. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye kurehemu.
إِنَّ شَجَرَتَ الزَّقُّومِ ( 43 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 43
Hakika Mti wa Zaqqum,
طَعَامُ الْأَثِيمِ ( 44 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 44
Ni chakula cha mwenye dhambi.
كَالْمُهْلِ يَغْلِي فِي الْبُطُونِ ( 45 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 45
Kama shaba iliyo yayushwa, hutokota matumboni
كَغَلْيِ الْحَمِيمِ ( 46 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 46
Kama kutokota kwa maji ya moto.
خُذُوهُ فَاعْتِلُوهُ إِلَىٰ سَوَاءِ الْجَحِيمِ ( 47 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 47
(Itasemwa:) Mkamateni na mtupeni katikati ya Jahannamu!
ثُمَّ صُبُّوا فَوْقَ رَأْسِهِ مِنْ عَذَابِ الْحَمِيمِ ( 48 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 48
Kisha mmwagieni juu ya kichwa chake adhabu ya maji yanayo chemka.
ذُقْ إِنَّكَ أَنتَ الْعَزِيزُ الْكَرِيمُ ( 49 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 49
Onja! Ati wewe ndiye mwenye nguvu, mtukufu!
إِنَّ هَٰذَا مَا كُنتُم بِهِ تَمْتَرُونَ ( 50 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 50
Hakika haya ndiyo mliyo kuwa mkiyatilia shaka.
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي مَقَامٍ أَمِينٍ ( 51 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 51
Hakika wachamngu watakuwa katika mahali pa amani,
فِي جَنَّاتٍ وَعُيُونٍ ( 52 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 52
Katika mabustani na chemchem,
يَلْبَسُونَ مِن سُندُسٍ وَإِسْتَبْرَقٍ مُّتَقَابِلِينَ ( 53 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 53
Watavaa hariri nyepesi na hariri nzito wakikabiliana,
كَذَٰلِكَ وَزَوَّجْنَاهُم بِحُورٍ عِينٍ ( 54 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 54
Hivi ndivyo itakavyo kuwa, na tutawaoza mahurilaini.
يَدْعُونَ فِيهَا بِكُلِّ فَاكِهَةٍ آمِنِينَ ( 55 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 55
Humo watataka kila aina ya matunda, na wakae kwa amani.
لَا يَذُوقُونَ فِيهَا الْمَوْتَ إِلَّا الْمَوْتَةَ الْأُولَىٰ ۖ وَوَقَاهُمْ عَذَابَ الْجَحِيمِ ( 56 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 56
Humo hawataonja mauti ila mauti yale ya kwanza, na (Mwenyezi Mungu) atawalinda na adhabu ya Jahannamu,
فَضْلًا مِّن رَّبِّكَ ۚ ذَٰلِكَ هُوَ الْفَوْزُ الْعَظِيمُ ( 57 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 57
Kuwa ni fadhila zitokazo kwa Mola wako Mlezi. Huko ndiko kufuzu kukubwa.
فَإِنَّمَا يَسَّرْنَاهُ بِلِسَانِكَ لَعَلَّهُمْ يَتَذَكَّرُونَ ( 58 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 58
Basi tumeifanya nyepesi hii Qur'ani kwa ulimi wako, ili wapate kukumbuka.
فَارْتَقِبْ إِنَّهُم مُّرْتَقِبُونَ ( 59 ) Ad-Dukhan ( The Smoke ) - Ayaa 59
Ngoja tu, na wao wangoje pia.

Random Books

Choose language

Choose Sorah

Random Books

Choose tafseer

Participate

Bookmark and Share