Swahili - Sorah An-Naba' ( The Great News )

Noble Quran » Swahili » Sorah An-Naba' ( The Great News )

Choose the reader


Swahili

Sorah An-Naba' ( The Great News ) - Verses Number 40
عَمَّ يَتَسَاءَلُونَ ( 1 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 1
WANAULIZANA nini?
عَنِ النَّبَإِ الْعَظِيمِ ( 2 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 2
Ile khabari kuu,
الَّذِي هُمْ فِيهِ مُخْتَلِفُونَ ( 3 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 3
Ambayo kwayo wanakhitalifiana.
كَلَّا سَيَعْلَمُونَ ( 4 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 4
La! Karibu watakuja jua.
ثُمَّ كَلَّا سَيَعْلَمُونَ ( 5 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 5
Tena la! Karibu watakuja jua.
أَلَمْ نَجْعَلِ الْأَرْضَ مِهَادًا ( 6 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 6
Kwani hatukuifanya ardhi kama tandiko?
وَالْجِبَالَ أَوْتَادًا ( 7 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 7
Na milima kama vigingi?
وَخَلَقْنَاكُمْ أَزْوَاجًا ( 8 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 8
Na tukakuumbeni kwa jozi?
وَجَعَلْنَا نَوْمَكُمْ سُبَاتًا ( 9 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 9
Na tukakufanya kulala kwenu ni mapumziko?
وَجَعَلْنَا اللَّيْلَ لِبَاسًا ( 10 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 10
Na tukaufanya usiku ni nguo?
وَجَعَلْنَا النَّهَارَ مَعَاشًا ( 11 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 11
Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia maisha?
وَبَنَيْنَا فَوْقَكُمْ سَبْعًا شِدَادًا ( 12 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 12
Na tukajenga juu yenu saba zenye nguvu?
وَجَعَلْنَا سِرَاجًا وَهَّاجًا ( 13 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 13
Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto;
وَأَنزَلْنَا مِنَ الْمُعْصِرَاتِ مَاءً ثَجَّاجًا ( 14 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 14
Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni,
لِّنُخْرِجَ بِهِ حَبًّا وَنَبَاتًا ( 15 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 15
Ili tutoe kwayo nafaka na mimea,
وَجَنَّاتٍ أَلْفَافًا ( 16 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 16
Na mabustani yenye miti iliyo kamatana.
إِنَّ يَوْمَ الْفَصْلِ كَانَ مِيقَاتًا ( 17 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 17
Hakika siku ya uamuzi imewekewa wakati wake,
يَوْمَ يُنفَخُ فِي الصُّورِ فَتَأْتُونَ أَفْوَاجًا ( 18 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 18
Siku litapo pulizwa barugumu, nanyi mtakuja kwa makundi,
وَفُتِحَتِ السَّمَاءُ فَكَانَتْ أَبْوَابًا ( 19 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 19
Na mbingu zitafunguliwa, ziwe milango,
وَسُيِّرَتِ الْجِبَالُ فَكَانَتْ سَرَابًا ( 20 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 20
Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi.
إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتْ مِرْصَادًا ( 21 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 21
Hakika Jahannamu inangojea!
لِّلطَّاغِينَ مَآبًا ( 22 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 22
Kwa walio asi ndio makaazi yao,
لَّابِثِينَ فِيهَا أَحْقَابًا ( 23 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 23
Wakae humo karne baada ya karne,
لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرْدًا وَلَا شَرَابًا ( 24 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 24
Hawataonja humo chochote kibaridi wala kinywaji,
إِلَّا حَمِيمًا وَغَسَّاقًا ( 25 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 25
Ila maji yamoto sana na usaha,
جَزَاءً وِفَاقًا ( 26 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 26
Ndio jaza muwafaka.
إِنَّهُمْ كَانُوا لَا يَرْجُونَ حِسَابًا ( 27 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 27
Hakika hao hawakuwa wakitaraji kuwa kuna hisabu.
وَكَذَّبُوا بِآيَاتِنَا كِذَّابًا ( 28 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 28
Na wakikanusha Aya zetu kwa nguvu.
وَكُلَّ شَيْءٍ أَحْصَيْنَاهُ كِتَابًا ( 29 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 29
Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika.
فَذُوقُوا فَلَن نَّزِيدَكُمْ إِلَّا عَذَابًا ( 30 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 30
Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!
إِنَّ لِلْمُتَّقِينَ مَفَازًا ( 31 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 31
Hakika wachamngu wanastahiki kufuzu,
حَدَائِقَ وَأَعْنَابًا ( 32 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 32
Mabustani na mizabibu,
وَكَوَاعِبَ أَتْرَابًا ( 33 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 33
Na wake walio lingana nao,
وَكَأْسًا دِهَاقًا ( 34 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 34
Na bilauri zilizo jaa,
لَّا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا كِذَّابًا ( 35 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 35
Hawatasikia humo upuuzi wala uwongo -
جَزَاءً مِّن رَّبِّكَ عَطَاءً حِسَابًا ( 36 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 36
Malipo kutoka kwa Mola wako Mlezi, kipawa cha kutosha.
رَّبِّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا الرَّحْمَٰنِ ۖ لَا يَمْلِكُونَ مِنْهُ خِطَابًا ( 37 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 37
Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilio baina yao, Arrahman, Mwingi wa rehema; hawamiliki usemi mbele yake!
يَوْمَ يَقُومُ الرُّوحُ وَالْمَلَائِكَةُ صَفًّا ۖ لَّا يَتَكَلَّمُونَ إِلَّا مَنْ أَذِنَ لَهُ الرَّحْمَٰنُ وَقَالَ صَوَابًا ( 38 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 38
Siku atakapo simama Roho na Malaika kwa safu. Hawatasema ila Mwingi wa rehema aliye mruhusu, na atasema yaliyo sawa tu.
ذَٰلِكَ الْيَوْمُ الْحَقُّ ۖ فَمَن شَاءَ اتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِ مَآبًا ( 39 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 39
Hiyo ndiyo Siku ya haki. Basi anaye taka na ashike njia arejee kwa Mola wake Mlezi.
إِنَّا أَنذَرْنَاكُمْ عَذَابًا قَرِيبًا يَوْمَ يَنظُرُ الْمَرْءُ مَا قَدَّمَتْ يَدَاهُ وَيَقُولُ الْكَافِرُ يَا لَيْتَنِي كُنتُ تُرَابًا ( 40 ) An-Naba' ( The Great News ) - Ayaa 40
Hakika tumekuhadharisheni adhabu iliyo karibu kufika; Siku ambayo mtu atakapo ona yaliyo tangulizwa na mikono yake; na kafiri atasema: Laiti ningeli kuwa udongo!

Random Books

Choose language

Choose Sorah

Random Books

Choose tafseer

Participate

Bookmark and Share